Muundo wa Insha
Kwa kawaida insha inakuwa na sehemu kuu nne:
kichwa cha insha, utangulizi, kiini na hitimisho.
a.
Kichwa cha insha;Kichwa cha insha hudokeza kile utachokijadili
katika insha yako, hubainisha wazo kuu la mada inayohusika. Kwa kawaida kichwa
cha insha huandikwa kwa sentensi fupi. Mfano; maisha ya kijijini, mimba za
utotoni.
b.
Utangulizi;Mambo yaliyopo katika utangulizi ni pamoja na kutoa fasili ya
maneno muhimu na kuelezea kwa muhtasari mambo ambayo utakwenda kuyajadili
katika insha yako. Utangulizi unakuwa katika aya moja fupi.
c.
Kiini cha insha; Katika kiini ndipo kuna maelezo ya kina juu
ya kile unachokijadili katika insha yako, maelezo haya yanakuwa katika aya
kadhaa kulingana na idadi ya hoja ulizonazo katika mjadala wako.
d.
Hitimisho; Hapa ndipo kuna muhtasari wa kile kilichojadiliwa katika kiini
cha insha au inaweza kuwa ni msimamo juu ya kile kilichojadiliwa katika insha.
No comments:
Post a Comment